TIMU YA SIMBA NA YANGA ZA ZUILIWA KUUTUMIA UWANJA WA TAIFA...
Hii ni kufuatia uharibifu uliofanyika katika Mechi zao zilizochezwa October 1, 2016 ikiwa katika Mechi hiyo Simba na Yanga timu zote zilitoka zikiwa na sare ya bao 1-1. Mhe waziri wa michezo Nape Nauye alitembelea uwanja huo wa Taifa na kuona uharibifu huo na kutoa kauli ya Simba na Yanga hawaruhusiwi kuchezea mechi zake hapo mpaka hapo baadae watakapoambiwa.