MSHINDI WA BSS MWAKA JANA 2015 KAYUMBA AELEZA HAYA JUU MATUMIZI YA HELA YAKE...
Ni msanii kutoka katika Zao la Bongo Star Search 2015, Kayumba Juma amefunguka kueleza namna milioni 50 alizoshinda kwenye Shindano la Bongo Star Search zilivyotumika.
Msanii huyo amefunguka haya na kusema "Kiasi nilichokichukua kilikuwa ni milioni 50 ambazo zimetumika katika matumizi yangu ambapo sasa hivi niko kwenye ujenzi wa Nyumba yangu mpya iliyopo maeneo ya Mbagala, na pia nimenunua usafiri wangu mpya wa kuzunguka hapa na pale kwenda Studio na sehemu zingine"- Kayumba